HATARI
ZA DAWA ZA NGUVU ZA KIUME ZENYE KEMIKALI
Tatizo
la nguvu za kiume linalowaathiri mamilioni ya watu na pia kuathiri mahusiano ya
kimapenzi .Katika kazi yangu katika Cliniki ya Afya ya Mapenzi asilimia 97% ya
wateja wangu ni wanaume na leo nimeona nizungumzie hatari za kutumia madawa
mengine yauzwayo katika maduka ya madawa mbalimbali.
Nimeamua
kuandika habari hizi baada ya kaka mmoja aliesafiri toka Tabora na kuja kuniona
baada ya kwenda katika hospitali ya moja ya rufaa akiwa na tatizo la kuwahi kumaliza bila kupata
msaada. Tatizo hilo limekuwa kero kwa mke wake na hivyo kutaka kuliondoa kwa
gharama yeyote ile. Kaka huyo alienda kwa Daktari bingwa wa mambo ya uume na uke na mambo ya viungo vya uzazi kwa
kitaalamu wanaitwa UROLOGISTS.
Baada
ya kuelezea tatizo lake kwa Daktari huyo bingwa alipewa dawa ambazo ni kwa tatizo
la nguvu za kiume na hazikumsaidia katika tatizo lake. Nilishangaa kusikia kuwa
Daktari bingwa ameshindwa kumsaidia kaka huyo kwani tayari huyo kaka alikuwa
anafahamu madhara ya dawa hizo na hivyo kwa kuwa alikuwa tayari amekwisha sikia
katika vipindi vyangu vya redio vya USIKU WA MAHABA siku ya Jumatano katika
redio FREE AFRIKA alinitafuta alikuja kwangu kama hatua ya mwisho katika
mahangaiko yake.Nilifanikiwa kumsaidia na tatizo lake likawa ni historia.
Mwanzoni
mwa kazi yangu 2006 nilikuwa nawapa watu dawa hizo zinazouzwa madukani na siku
moja Mzee mmoja anaefanya kazi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jijini Mwanza
alikuja na malalamiko yanayofanana kabisa na kaka huyo toka Tabora. Nilimweleza
juu ya tiba mbili nilizonazo yaani dawa hizo za madukani zinazokupa nguvu ya
masaa 4 na dawa yangu ya asili inayoweza kukuondolea tatizo hilo baada ya siku
5 hadi 7. Baba huyo akachagua dawa hiyo
ya haraka akaitumia siku hiyo hiyo ili kumziba mdomo mke wake.
Nilimuuzia
dawa hizo baba huyo mwenye umri wa miaka 46 na alienda na kuzitumia hizo dawa.
Kesho yake baba huyo alirudi ofisini kwangu na kuniambia kuwa kweli alifanikiwa
kumfurahisha mke wake usiku uliopita lakini majira ya saa 9 usiku aliamshwa na
maumivu makali ya kichwa na kuiona dunia yote kuwa ni rangi ya njano.
Nisingependa upate matatizo yanayofanana na
hayo na yafuatayo ni uthibitisho wa kisayansi wa madhara ya dawa hizo:-
Kuna
tovuti 22 milioni zinazoshabikia madawa mbalimbali ya nguvu za kiume zenye
kemikali za hatari kwako kwa hiyo ni
rahisi kushawishiwa na kutapeliwa. Shirika la kudhibiti madawa na vyakula la huko Marekani
limeorodhesha majina ya madawa yenye
madhara kwa mtumiajo na madawa hayo ni Zimayx, vigor – 25, True Man ,Shanghai
Ultra, neophase, Nasutra Man up now, Liviro 3 , Libidus, Lady Shanghai, Hs joy
of love, Energy Max, Blue steel, Actva Sx ,Activa Rx na Adam free.
Madawa
hayo yote na mengineyo yasioorodheshwa hapo hufanya kazi kama ifuatavyo:-
Madawa
hayo yana kemikali iitwayo PHOSIPHODIESTERASE 51 (PDE51) na kazi ya PDE51 ni
kuzuia nguvu ya Enzyme iitwayo PHOSPHODIESTERASE 5 (PDE5)ambayo ndiyo inayozuia
uume kusimama kama inavyotakiwa. Kemikali ya PDE51 inanyonywa ndani ya
damu na ndani ya saa moja mwanaume anakuwa
na nguvu ya kumuwezesha kushiriki tendo la ndoa ndani ya masaa yasiozidi 4
kutokana na afya ya mtu mara nyingi
nguvu za dawa hiyo huweza kwenda hadi
masaa 7.
Ubaya
wa madawa hayo na mengine ni kwamba yana
kemikali iitwayo GLYBURIDE yenye nguvu ya kuathiri mapigo ya moyo na kushusha
presha ya damu ambayo ni hatari sana. Mwaka 2008 huko mjini Singapore watu 150
walilazwa hospitalini kutokana na kutumia madawa hayo.
Shirika
la kuthibiti madawa la Marekani la FDA lilifanya upelelezi na kugundua kuwa
madawa mengi ya nguvu za kiume yana kemikali ambazo ni za hatari.
Dalili
za kuwa umeanza kuathirika na madawa hayo UNAPOZITUMIA ni hizi zifuatazo:-
(1)
Maumivu ya misuli.
(2)
Kupata shida ya upumuaji.
(3)
Maumivu ya kichwa.
(4)
Maumivu ya macho au kulegea kwa macho.
(5)
Kupiga chafya ovyo ovyo.
(6)
Kuvurugika kwa tumbo mara baada ya kula
chakula.
(7)
Mafua.
(8)
Kupata shida kupata usingizi.
(9)
Ngozi kuwa na joto lisilo la kawaida.
(10)
Maumivu ya masikio.
(11)
Kichefuchefu.
(12)
Ulimi kuwa mwekundu kuliko kawaida.
(13)
Kushindwa kumwaga mbegu hata ukifanya tendo
la ndoa kwa muda mrefu.
(14)
Kuona dunia imebadilika rangi.
(15)
Kuwa na hali ya wasiwasi bila ya sababu
yeyote.
(16)
Maumivu kifuani.
(17)
Kutokuona sawa sawa.
(18)
Njaa ya kupita kiasi.
(19)
Kuongezeka kwa ukubwa wa mboni ya jicho.
(20)
Kutokwa jasho sana.
(21)
Maumivu ya mgongo.
(22)
Kutopendelea mwanga mkali.
(23)
Uchovu wa bila sababu.
Ndugu
nimeandika hayo kufumbua macho uone kwa yapo madhara na ukitaka uhakika iwapo
unafahamu kiingereza tafuta kwenye GOOGLE kwa kuandika ED drugs are harmful na utajionea mwenyewe ukweli huo.
Dawa
ya PRIKA utakayoiona katika blog hii ni ya asilia kwani imetokana na mimea
halisi na haifanyi kazi mpaka imetanguliwa na mazoezi maalumu utakayofanya
ukiwa umekaa kwenye kiti. Uanzapo kutumia dawa hii ya PRIKA utaanza kuona
mabadiliko baada ya siku 5 – 7 lakini utaitumia dawa hiyo kwa wiki mbili ili
kulifuta tatizo la nguvu za kiume na la kuwahi kumaliza .Unapoagiza dawa hiyo
utapewa kijarida kitakachokupa maelekezo ya kutumia dawa hiyo na pia maelekezo
ya mambo ya kuepuka ili tatizo hilo lisikurudie tena maisha yako yote.