Thursday, November 13, 2014

HATARI ZA DAWA ZA NGUVU ZA KIUME ZENYE KEMIKALI

Tatizo la nguvu za kiume linalowaathiri mamilioni ya watu na pia kuathiri mahusiano ya kimapenzi .Katika kazi yangu katika Cliniki ya Afya ya Mapenzi asilimia 97% ya wateja wangu ni wanaume na leo nimeona nizungumzie hatari za kutumia madawa mengine yauzwayo katika maduka ya madawa mbalimbali.

Nimeamua kuandika habari hizi baada ya kaka mmoja aliesafiri toka Tabora na kuja kuniona baada ya kwenda katika hospitali ya moja ya rufaa  akiwa na tatizo la kuwahi kumaliza bila kupata msaada. Tatizo hilo limekuwa kero kwa mke wake na hivyo kutaka kuliondoa kwa gharama yeyote ile. Kaka huyo alienda kwa Daktari bingwa wa mambo ya  uume na uke na mambo ya viungo vya uzazi kwa kitaalamu  wanaitwa UROLOGISTS.

Baada ya kuelezea tatizo lake kwa Daktari huyo bingwa alipewa dawa ambazo ni kwa tatizo la nguvu za kiume na hazikumsaidia katika tatizo lake. Nilishangaa kusikia kuwa Daktari bingwa ameshindwa kumsaidia kaka huyo kwani tayari huyo kaka alikuwa anafahamu madhara ya dawa hizo na hivyo kwa kuwa alikuwa tayari amekwisha sikia katika vipindi vyangu vya redio vya USIKU WA MAHABA siku ya Jumatano katika redio FREE AFRIKA alinitafuta alikuja kwangu kama hatua ya mwisho katika mahangaiko yake.Nilifanikiwa kumsaidia na tatizo lake likawa ni historia.

Mwanzoni mwa kazi yangu 2006 nilikuwa nawapa watu dawa hizo zinazouzwa madukani na siku moja Mzee mmoja anaefanya kazi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jijini Mwanza alikuja na malalamiko yanayofanana kabisa na kaka huyo toka Tabora. Nilimweleza juu ya tiba mbili nilizonazo yaani dawa hizo za madukani zinazokupa nguvu ya masaa 4 na dawa yangu ya asili inayoweza kukuondolea tatizo hilo baada ya siku 5 hadi 7.  Baba huyo akachagua dawa hiyo ya haraka akaitumia siku hiyo hiyo ili kumziba mdomo mke wake.

Nilimuuzia dawa hizo baba huyo mwenye umri wa miaka 46 na alienda na kuzitumia hizo dawa. Kesho yake baba huyo alirudi ofisini kwangu na kuniambia kuwa kweli alifanikiwa kumfurahisha mke wake usiku uliopita lakini majira ya saa 9 usiku aliamshwa na maumivu makali ya kichwa na kuiona dunia yote kuwa ni rangi ya njano.
 Nisingependa upate matatizo yanayofanana na hayo na yafuatayo ni uthibitisho wa kisayansi wa madhara ya dawa hizo:-

Kuna tovuti 22 milioni zinazoshabikia madawa mbalimbali ya nguvu za kiume zenye kemikali za hatari kwako  kwa hiyo ni rahisi kushawishiwa na kutapeliwa. Shirika la  kudhibiti madawa na vyakula la huko Marekani limeorodhesha  majina ya madawa yenye madhara kwa mtumiajo na madawa hayo ni Zimayx, vigor – 25, True Man ,Shanghai Ultra, neophase, Nasutra Man up now, Liviro 3 , Libidus, Lady Shanghai, Hs joy of love, Energy Max, Blue steel, Actva Sx ,Activa Rx na Adam free.

Madawa hayo yote na mengineyo yasioorodheshwa hapo hufanya kazi kama ifuatavyo:-
Madawa hayo yana kemikali iitwayo PHOSIPHODIESTERASE 51 (PDE51) na kazi ya PDE51 ni kuzuia nguvu ya Enzyme iitwayo PHOSPHODIESTERASE 5 (PDE5)ambayo ndiyo inayozuia uume kusimama kama inavyotakiwa. Kemikali ya PDE51 inanyonywa ndani ya damu  na ndani ya saa moja mwanaume anakuwa na nguvu ya kumuwezesha kushiriki tendo la ndoa ndani ya masaa yasiozidi 4 kutokana na afya ya mtu mara  nyingi nguvu za dawa hiyo huweza kwenda hadi  masaa 7.

Ubaya wa madawa hayo  na mengine ni kwamba yana kemikali iitwayo GLYBURIDE yenye nguvu ya kuathiri mapigo ya moyo na kushusha presha ya damu ambayo ni hatari sana. Mwaka 2008 huko mjini Singapore watu 150 walilazwa hospitalini kutokana na kutumia madawa hayo.

Shirika la kuthibiti madawa la Marekani la FDA lilifanya upelelezi na kugundua kuwa madawa mengi ya nguvu za kiume yana kemikali ambazo ni za hatari.

Dalili za kuwa umeanza kuathirika na madawa hayo  UNAPOZITUMIA ni hizi zifuatazo:-

(1)        Maumivu ya misuli.
(2)        Kupata shida ya upumuaji.
(3)        Maumivu ya kichwa.
(4)        Maumivu ya macho au kulegea kwa macho.
(5)        Kupiga chafya ovyo ovyo.
(6)        Kuvurugika kwa tumbo mara baada ya kula chakula.
(7)        Mafua.
(8)        Kupata shida kupata usingizi.
(9)        Ngozi kuwa na joto lisilo la kawaida.
(10)     Maumivu ya masikio.
(11)     Kichefuchefu.
(12)     Ulimi kuwa mwekundu kuliko kawaida.
(13)     Kushindwa kumwaga mbegu hata ukifanya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
(14)     Kuona dunia imebadilika rangi.
(15)     Kuwa na hali ya wasiwasi bila ya sababu yeyote.
(16)     Maumivu kifuani.
(17)     Kutokuona sawa sawa.
(18)     Njaa ya kupita kiasi.
(19)     Kuongezeka kwa ukubwa wa mboni ya jicho.
(20)     Kutokwa jasho sana.
(21)     Maumivu ya mgongo.
(22)     Kutopendelea mwanga mkali.
(23)     Uchovu wa bila sababu.


Ndugu nimeandika hayo kufumbua macho uone kwa yapo madhara na ukitaka uhakika iwapo unafahamu kiingereza tafuta kwenye GOOGLE kwa kuandika ED drugs are harmful na utajionea mwenyewe ukweli huo.


Dawa ya PRIKA utakayoiona katika blog hii ni ya asilia kwani imetokana na mimea halisi na haifanyi kazi mpaka imetanguliwa na mazoezi maalumu utakayofanya ukiwa umekaa kwenye kiti. Uanzapo kutumia dawa hii ya PRIKA utaanza kuona mabadiliko baada ya siku 5 – 7 lakini utaitumia dawa hiyo kwa wiki mbili ili kulifuta tatizo la nguvu za kiume na la kuwahi kumaliza .Unapoagiza dawa hiyo utapewa kijarida kitakachokupa maelekezo ya kutumia dawa hiyo na pia maelekezo ya mambo ya kuepuka ili tatizo hilo lisikurudie tena maisha yako yote.

No comments:

Post a Comment