KANUNI
MUHIMU KWA WANAWAKE
(1)
Kuwa
mwanamke ambaye anahitajiwa na mwanaume na sio mwanamke anayehitaji mwanaume.
Tafsiri
yake
Kibaologia ubongo wa mwanaume una tofauti kubwa
ukilinganisha na wa mwanamke na hivyo utendaji wao na mahitaji yao yana
utofauti pia. Uwezo wa kuzungumza wa mwanamke ni mkubwa kuliko wa mwanaume,
yaani kwa siku moja mwanamke ana uwezo wa kuongea maneno 20,000 wakati mwanaume
ana uwezo wa kuongea maneno 7,000 kwa siku. Mwanamke asipojua njia za kuoanisha
tofauti hizi atamchukiza mwanaume bila ya yeye kujua na ndio maana Biblia
inasema “kila mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake. Bali aliyempumbavu
huibomoa kwa mikono yake mwenyewe (Mithali 14:1).Ili uweze kuwa mwanamke ambaye
mwanaume anamhitaji inakupasa usome mahitaji ya mwanaume vizuri ili uweze
kuyatimiza kikamilifu na kumtosheleza kabisa.
(2)
Mwanaume
akikuacha au kukudharau ni hasara yake na sio yako.
Tafsiri
yake
Iwapo una uhakika wa kuifuata vizuri kanuni ya kwanza
na kwa bahati mbaya ukapata mwanaume asieuona uthamani wako usibabaike kabisa.
Yeye ndie kipofu haoni thamani yako na kuandoka kwake toka katika maisha yako
maana yake Mungu anakuelekeza kwa mwanaume mwingine aliye bora kuliko huyo.
Biblia inakuagiza “Tulia ujue ya kuwa mimi ni Mungu nitatukuzwa katika mataifa”
Zaburi 46:10.
(3)
Onekana
kama kipepeo lakini ng’ata kama nyuki.
Tafsiri
yake
Biblia inasema kwamba wanawake wanapaswa wajipambe kwa
utu wa moyoni usioonekana yaani roho ya upole na utulivu na hekima (Petro 3:4).
Mwanamke pamoja na mapambo yote na uzuri wa nje ni muhimu tabia yake ionyeshe
utulivu na upole. Kipepeo haumizi mtu na anapendeza kwa muonekano wake lakini
hivyo peke yake haitoshi kuvuta na kutunza penzi la mwanaume. Hivyo basi ni
muhimu mwanamke mara nyingine awe kama nyuki, yaani aonyeshe ukali pale anapoonelewa.
Ajenge uwezo wa kuelezea hisia zake bila ya uoga wowote ule.KUMBUKA kuwa
wanaume hupenda wanawake wanaoleta changamoto zinazojenga na sio wenye unafiki.
Kwa kufanya hivyo ataweza kudumisha penzi katika msingi
wa haki na ukweli na sio unafiki. Fuata maneno ya BWANA YESU “kuweni na busara kama
nyoka na wapole kama njiwa (Mt 10:16).
(4)
Usianzishe ugomvi bali zifahamu njia
za kumaliza ugomvi
Tafsiri
Ukiwa mpole utapenda sana kutafuta kumwelewa mwenzio
badala ya kumhukumu ,ukimhukumu hasira huja haraka na hivyo kuanzisha ugomvi.
Epuka kukurupuka na kusema maneno harakaharaka .Jifunze kutulia japo umeumia au
kukasirika. Kwa kufanya hivyo utaweza kuona kwa urahisi njia za kujibu na
kutatua migogoro katika mahusiano yako.
(5)
Kuwa mpenzi na sio mpiganaji lakini
siku zote pigania unachokipenda
Tafsiri
Unapoamua kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu jitahidi
kumpa mapenzi yote kwa moyo wote. Pamoja na hayo yote yatokeapo magumu kuwa
mstaarabu kuepuka hali ya ugomvi kwa kujizuia kupaza sauti au kuongea maneno
makali. Jambo la msingi tambua mambo muhimu na usikubali mpenzi wako ayapuuzie
mambo hayo kwa urahisi. Jenga hoja nzito za kupigania haki yako ya kuishi
maisha ya furaha na amani.
(6)
Kupata
kitu ambacho hujawahi kukipata ni lazima ufanye vitu ambavyo hujawahi kufanya.
Tafsiri
Ni rahisi sana kufanya vitu ulivyozoea na kufurahia
hali hiyo mpaka pale itakapotokea shida fulani inayohusiana na kitu ulichokizoea .Ili uweze
kuendelea kufurahia uhusiano wako zaidi ni muhimu utafute vitu vipya vya
kupamba na kuimarisha uhusiano wako. Hapa inahitaji ubunifu, uchunguzi na
ujasiri wa kujaribu jambo ambalo hujawahi kukutana nalo. Kwa kuwa kila siku
tunakutana na mambo mengi upo uwezekano mkubwa wa mtu kubadili mtazamo wake juu
yako na ukapata matatizo katika uhusiano wako. Kuleta vitu vipya huleta
msisimko mkubwa na iwapo wewe ndio utakuwa chanzo cha msisimko huo basi
utathaminiwa na kupendwa zaidi.
(7)
Kabla hujauliza kwanini fulani
hakupendi, jiulize kwanini unajali sana juu ya hilo.
Tafsiri
Kumpenda mtu mwingine ni kitu rahisi sana na sisi wote
tumo katika kundi hilo lakini kumfanya mtu mwingine akupende au aendelee kukupenda sio rahisi kabisa.Pale
unapotamani mtu fulani akupende kwanza jiangalie mwenyewe vizuri je kama mtu
huyo anapenda mtu mwenye maumbile mazuri unayo sifa hiyo?. Kama anapenda mtu
mfupi wewe unayo sifa hiyo? Na kama anataka mtu mwenye elimu au mwenye pesa
wewe umo kwenye kundi hilo.? Hayo yanaweza kuwa maswali magumu kwa wengi lakini
swali lingine rahisi kwa kila mtu ni je ni kwa vipi mimi nitaweza kuchangia
furaha yake zaidi ya mtu mwingine yoyote?. Ukiweza kujibu swali hili unanafasi
kubwa ya kujisogeza kwake na yeye akakuona kuwa kweli unafaa, lakini
ukijisogeza bila kuwa na sifa za kutosha unatafuta maumivu ya moyo. Madhaifu
kama aibu, hasira, woga, unene kupita kiasi, uvivu au kupenda kuongea bila ya
kuchoka yanaweza kuharibu penzi hata kama utapata mtu mwenye penzi la kweli.
Jichunguze kama vile Biblia isemavyo.“ Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na
angalia asianguke (1Wakorintho 10:12)
“Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani,
jithibitisheni wenyewe (2 Wakorintho 13:5).